WAZIRI MKUU AGAWA MIPIRA, JEZI ZA SOKA WILAYANI MPANDA

Friday, May 15, 2009

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

WAZIRI MKUU AGAWA MIPIRA, JEZI ZA SOKA WILAYANI MPANDA

WAZIRI MKUU Mizengo Pinda ametoa mipira 13 na seti 16 za jezi za mpira wa miguu kwa kata za wilaya ya Mpanda ambazo zimetolewa na kampuni ya simu ya VODACOM.

Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo kutoka kwa Meneja wa Vodacom kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Bw. Jackson Kiswaga, Waziri Mkuu alisema ameamua kugawa jezi hizo na mipira katika wilaya nzima ili kuimarisha michezo wilayani humo.

Alisema ameamua kuwaita wadau kutoka majimbo yote matatu ya wilaya hiyo ili wao ndiyo waamue jinsi ya kugawana kwa vipaumbele kwani wilaya nzima ina kata 29 lakini vifaa vilivyopatikana vitatosha kata 16 tu.

“Ninawomba Mwenyekiti na Meya kila mmoja akae na wadau wake na kuangalia njia muafaka ya kugawana hicho kidogo kilichopatikana,” alisema

Alisema ameamua kutoa jezi seti tano na mipira saba kwa ajili ya jimbo la Mpanda Magharibi ambako kuna kata saba; seti nyingine tano za jezi na mipira sita kwa jimbo la Mpanda Kati ambako kuna kata sita na jezi seti sita zilizobaki zitagawiwa jimbo la Mpanda Mashariki ambalo ni la kwake na lina kata 16. Hakuna mipira iliyotolewa kwa jimbo hili.

“Nimeongea na Mkuu wao, na kuwaomba watusaidie kwa ajili ya kata hiyo 13 zilizobaki, wamekubali kwa hiyo itabidi hizo kata nyingine zisubiri hadi tutakapoambiwa mambo ni tayari,” alisema.

Akizungumza katika hafla hiyo fupi iliyofanyika Ikulu ndogo mjini Mpanda, Bw. Kiswaga alisema walikubali kutoa msaada huo kwa sababu wanamfahamu Waziri Mkuu Pinda kama mtu ambaye amekuwa akiendesha mashindano ya mpira mara kwa mara ili kudumisha umoja.

(mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
DAR ES SALAAM
IJUMAA, MEI 15, 2009.

0 comments:

Post a Comment

About This Blog

Blog Archive

  © Blogger template Noblarum by Ourblogtemplates.com 2009

Back to TOP